Monday, April 2, 2012

MTI JUU YA NYUMBA

Katika pitapita zangu nilishtushwa na huu mti ulioota juu ya nyumba hii ambayo inaishi watu kama kawa, wakazi wa nyumba hii wanaonekana kutokuwa na wasiwasi wowote juu ya mti huo ulioota juu ya nyumba yao. Baada ya kumhoji mmoja wa wakazi wa nyumba hiyo alisema kwamba wao hawana hofu yoyote kuhusu mti huo kutokana na kuamini uimara wa nyumba yao.

Monday, March 19, 2012

AJALI KAZINI.......

Usalama barabarani hapo vip?

HII NDIO TANZANIA

Saturday, October 22, 2011

JAMANI MAISHA HAYA !!!!!....HILI NDIO JENGO LA STUDIO YA 6 RECORDS

Katika pita pita ya Leo kitaa nimelifumania jengo hili ambalo ndani ndio kuna studio bora ya mwaka ambayo ilijinyakulia tuzo ya Zanzibar Music Awards 2011. kilichinijia akilini ni kwamba ubora wa kazi si uzuri wa jengo naamini hata yule ambae amewahi kurekodi kazi yake analitambua hilo. Anaeonekana kwa mbali kama anaingia ndani hivi ni mmoja wa wasanii maarufu sana Znz Rico Single nae aliotewa pande hizo.
Studio ya 6 Rec ipo maeneo ya mwera lazima uvuke mto ukiwa umekunja suruali ama ubebwe kama we sharobaro upo? Nje ya studio hii kunalimwa mihogo,matembele,maboga na upupu pia nahisi utakuwepo.
Side 2 the Lee producer wa 6 rec