Sunday, April 26, 2015

Lady Jaydee ft. Mazet & Uhuru - GIVE ME LOVE

This is a brand new single from Lady Jaydee called "Give Me Love" featuring South Africa's Mazet and the Infamous Uhuru. Give me love, which is a follow up to her riddim driven smash hit 'Forever", is produced by Dj Maphorisa Uhuru. Be on the Look out for the Video which is slated to drop at the end of the month.

Thursday, April 23, 2015

Bongoflava Anthem 2015

Ni kipindi kirefu toka ngoma moja ikatuunganisha watanzania wote kwa pamoja, mwaka jana kulikuwa na Mwana ya Ali Kiba, Mwaka wa nyuma yake Number One ya Diamond na Mwaka huu hii ngoma kutoka kwa msanii KICHE LEGEND anayekuja kwa kasi juu. wimbo unaitwa Angalia Juu, ni wimbo wa celebration, ni hustlers anthem, ni wimbo mzuri kwa ujumla

SHIRIKA LA HOTELI YA WYNDHAM LAFUNGUA HOTELI YA KWANZA AFRIKA MASHARIKI

Ramada Resort yafunguliwa Dar es Salaam, Tanzania- Hoteli ya kwanza Afrika kuendeshwa na shirika la hoteli la Wyndham kwa mkataka ya usimamizi.
Shirika la Hoteli la Wyndham, ambalo linaongoza duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya hoteli na moja kati ya vitengo vitatu vya kibiashara vya Kampuni ya Wyndham Worldwide (http://www.wyndhamworldwide.com), leo limetangaza kufunguliwa kwa Ramada Resort yenye vyumba 139 jijini Dar es Salaam, Tanzania. Logo: http://www.photos.apo-opa.com/plog-content/images/apo/logos/whg.jpg Photo: http://www.photos.apo-opa.com/index.php?level=picture&id=1898 (Ramada Resort Dar es Salaam) Ufunguzi huu unaongezea kwenye hoteli nyingine nchini Morocco, Ghana, Nigeria na Tunisia, na kuendeleza upanuzi wa hoteli ya Wyndham katika kanda ya Afrika Mashariki. Pia hii ni hoteli ya kwanza AfriKa kuendeshwa kupitia kitengo cha usimamizi cha kampuni kinachoendelea kukua. “Ufunguzi wa Ramada Resort jijini Dar es Salaam una umuhimu mkubwa kimkakati kwetu” alisema Bw. Dan Ruff, ambaye ni Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa hoteli ya Wyndham katika eneo la Ulaya, Mashariki ya Kati, AfriKa na Bahari ya Hindi. Aliendelea kusema, “Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya malazi yenye ubora wa kimataifa katika Afrika Mashariki, pamoja na dhamira yetu ya kuwa karibu na wageni na wateja wetu kupitia upanuzi katika kitengo cha usimamizi wa mali, hii ni hatua muhimu sana katika ukuaji wetu katika kanda hii. " Pia Ruff alisema, “Ramada Resort ya Jijini Dar es Salaam, yenye vifaa vya kipekee na iliyoo kwenye eneo lenye mandhari mazuri ya ufukweni, imeweka viwango vipya kwa mahoteli yenye kiwango cha kati nchini Tanzania na tuna hamu ya kuwakaribisha wageni wetu wa kwanza kwa ukarimu wa kipekee wa Ramada” Kati ya jumla ya vyumba 139, vyumba 117 ni vyenye ubora mkubwa na viko mkabala na ufukwe au na bustani, vyumba 21 ni vya kiwango cha hadhi ya juu na chumba kimoja cha hadhi ya ‘presidential suite’. Vyumba vyote vina TV aina ya flatscreen na channel za satellite na mtandao wa Wi-Fi unapatikana bila malipo. Kadhalika, kuna baa ndogo, vifaa vya kukuwezesha kujitengenezea chai au kahawa na bafu binafsi vyumbani. Sanaa za michoro ya Tinga-tinga inaongezea mandhari ya Afrika mashariki. Vifaa vya burudani ni pamoja na bwawa la kuogelea, gym yenye vifaa vya kisasa na njia ya moja kwa moja inayoelekea ufukweni wa mchanga tifutifu. Kwa wateja wenye mikutano au matukio, tuna vyumba saba vya mikutano vinavyoweza kukaliwa na hadi watu 375 na maeneo matano ya vyakula na vinywaji yanayoandaa vyakula aina mbalimbali vya kiafrika na kimataifa vile vile. Tangu ujenzi ulipoanza 2009, tumezingatia mipango endelevu ikiwemo kutibu na kutumia upya asilimia 100 ya maji taka. Tumesistiza kutumia maji yaliyotumika kwa asilimia 100, matumizi ya nishati ya jua, kutumia mwanga wa taa za LED na ulinzi wa ufukwe ili usimommonyoke. Pia Hoteli inapanga jinsi ya kutumia mabaki ya chakula kama virutubisho kwa ajili ya kukuza mbogakwa ajili ya matumizi ya Hoteli, bustani hiyo iko katika Ghorofa ya juu kabisa ya Hoteli. Bw. Murtaza Fazal, mmiliki wa Ramada Dar Es Salaam, alisema “Ninafurahi kusaini mkataba wa muda mrefu na Wyndham Hotel Group, kampuni yenye Hoteli Kubwa duniani. Pia najivunia kuwa mwekezaji wa kwanza kuitambulisha Ramada katika soko la Afrika Mashariki. Ninaamini kuwa hii Ramada mpya iliyoko katika ufukwe wa Jangwani itakuwa ni kimbilio la wenyeji na hata watalii wa kimataifa na wageni wa kibiashara, tunajivunia mazingira bora, ubunifu na huduma bora. “Najivunia pia kuwa mwanzilishi wa matumizi ya nishati mbadala ili kulinda mazingira, ni matumaini yangu kuwa wamiliki wengine wa Hoteli watakuwa waiga mfano” Aliongeza Fazal,. Wageni watakaokaa katika hoteli ya Ramada Resort Dar es Salaam ambao ni wanachama wa Wyndham Rewards®, mpango wa kujiunga bure wa kuzawadia uaminifu wa wageni wa Ramada, wataweza kupata alama za thamani wakati wa ukaaji wao. Zawadi hizo ni kama vile malazi na chakula bila malipo, tiketi ya ndege bila malipo, kadi ya kufanya manunuzi na mengine mengi. Maelezo yanapatikana katika tovuti yetu, www.wyndhamrewards.com. Distributed by APO (African Press Organization) on behalf Wyndham Hotel Group. MAWASILIANO:Pegi AmarteifioPublicasityWyndham@publicasity.co.uk+44 20 3757 6800 Roz Money Wyndham Hotel Group The Triangle, 5 Hammersmith GroveLondon, W6 0LGUnited Kingdom +44 20 8762 6600roz.money@wyn.comWAHARIRI: Picha ziada na nembo zetu zinaweza kupatikana kutoka www.wyndhamhotelgroup/media . Kwa taarifa zaidi kuhusu Wyndham Worldwide Corporation na biashara zake, tembelea www.wyndhamworldwide.com . Kuhusu RamadaRamada Worldwide® ni sehemu ya kampuni ya hoteli za Wyndham na ina zaidi ya hoteli 830 duniani zenye ubora wa kati na wa juu. Hoteli hizi zinatoa huduma, ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa intaneti ya kasi ya Wi-Fi, migahawa, vyumba vya mapumziko, huduma za chumbani , huduma ya bawabu, huduma za mikutano na vyakula, vifaa na vituo vya biashara . Ramada pia inatoa fursa kwa wasafiri kupata na kukomboa pointi kwa njia ya Wyndham Rewards®, programu ya uaminifu wa wageni, ambayo wanaweza kujiunga bila malipo katika www.wyndhamrewards.com . Ramada aliadhimisha miaka 60 ya kuwepo kwake mwaka 2014. Kila hoteli ya Ramada inajitegemea kwa umiliki na uendeshwaji, isipokuwa kwa baadhi ya hoteli za Ramada zilizopo nje ya Marekani ambazo zinasimamiwa na wabia. Ramada Worldwide ni kampuni tanzu ya Wyndham Hotel Group na kampuni mzazi ya Wyndham Worldwide Corporation ( NYSE: Wyn ). Taarifa zaidi zinapatikana kwa kutembelea tovuti yetu www.ramada.com . Kuhusu Kampuni ya Hoteli za WyndhamKundi la Hoteli la Wyndham, ambalo linaongoza duniani kwa umiliki wa idadi ya hoteli na moja kati ya vitengo vitatu vya kibiashara vya Wyndham Worldwide (NYSE: WYN). Kampuni ya hoteli inayoongoza duniani ya Wyndham inamiliki takriban majengo 7,650 na vyumba 661,000 katika nchi 70 chini ya majina yafwatayo; Dolce Hotels and Resorts® (ilimilikiwa February 2015), Wyndham Grand® Hotels and Resorts, Wyndham Hotels and Resorts®, Wyndham Garden® Hotels, TRYP by Wyndham®, Wingate by Wyndham®, Hawthorn Suites by Wyndham®, Microtel Inn & Suites by Wyndham®, Ramada®, Ramada Encore®, Baymont Inn & Suites®, Days Inn®, Super 8®, Howard Johnson®, Travelodge® and Knights Inn®. Wyndham Rewards, programu ya uaminifu wa wageni imetoa nafasi kwa wateja zaidi ya milioni 38 kupata na kukomboa pointi katika maelfu ya hoteli duniani kote. Kwa taarifa zaidi temebelea tovuti yetu www.wyndhamworldwide.com. Safe Sender Instructions UNSUBSCRIBE

Wednesday, April 1, 2015

Shetta Ft Kcee - Shikorobo | Audio | Video

Hone Classic-We Mama (Official Video)


Follow @honeclassic Na utazame Official Video ya wimbo "We Mama" HAPA https://youtu.be/W3MbciIfKuk directed by @travellah toka Kwetu Studios, Co-starring @momoh_fyne_chic & @Jaqlynelameck alongside @fidovato pakua Audio HAPA https://mkito.com/song/we-mama/13233 by @defxtro @noizmekah na kwa mawasilano/mahojiano na HONE CLASSIC piga +255 767 861 349 powered by @mkitodotcom @vmgafrica www.vmgafrica.com #vmgafrica #SupportYourOwn

NEW MUSIC: Dom Down Click [DDC] Song: KIMENUKA [Audio]

NEW AUDIO: NICKRAY FT. KOKU - NIWEJE