Friday, July 27, 2012

PACKING YA MAGARI UWANJA WA NDEGE WA ZANZIBAR (AMANI INTER. AIRPORT) VUMBI TUPUUUU..

Hii ni njia ya kuingilia sehemu ya kusimamishia magari ya watu wanaokwenda kupokea wageni wao
Parking ya magari ya aina zote
Hili ndio eneo maalum la kusimamishia magari ya watu wanaokwenda kupokea wageni wao uwanja wa ndege wa Zanzibar (Amani International Air Port).
Endapo utakuwa umesimama eneo hili omba mungu kusije upepo mkali wa kunimua vumbi na endapo utakutana na upepo dakika kadhaa unapotezana na ndugu yako.

Habari isio rasmi kuna jamaa alienda kumpokea mpenzi wake alikuwa akitokea Uingereza alipotua uwanja wa ndege wa Zanzibar alikuwa amependeza sana alipokelewa na mpenzi wake vizuri wakakumbatiana sana kwa furaha, baada ya hapo walielekea liliko gari ambako ndio kama unavyoona kwenye picha hali ilivyo.

Basi baada ya kufika karibu na gari kulikuwa na watu wengi wametoka kupokea ndugu zao nao walikuwa wakijiandaa kuingia kwenye magari yao, hii ni june july upepo ni mkali wa kunimua vumbi ghafla ulipiga upepo ambao ulinimuwa vumbi kiasi cha kutoonana kama dakika 3 ulipokata ule upepokata kila mmoja alikuwa hamtambui mwenzie kwa jinsi sura zao zilivyokuwa kama vinyago yule mwanamke alipoambiwa na mpenzi wake ingia kwenye gari twende akamjibu kwani wewe ndio niliyekufuata akasisitiza kwani wewe ndio uliyekuja kunipokea we vipi embu achana na mimi hee jamaa alijua masihara kumbe mpenzi wake kamshau kwa jinsi alivyojaa vumbi na kuwa kama kinyago.

Serikali wananchi wanataka ile packing iwe saafi safi hata kama ni ya muda.

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako/ Leave your comments