Sunday, March 22, 2015

SITTI MTEMVU MGENI RASMI MAHAFALI YA UMOJA WA SHULE ZA SEC MOROGORO


Sitti A. Mtemvu mgeni rasmi katika mahafali ya umoja wa shule za sekondari Morogoro
Mh. Mariam Mtemvu akiongea na wanafunzi

Mariam Mtemvu akiwa na Sitti A Mtemvu wakifuatilia mahafali kwa makini ukumbini

Mgeni Rasmi akimkabidhiwa Risala kutoka kwa wanafunzi

Baadhi ya wanafunzi wahitimu wakimsikiliza mgeni Rasmi Sitti Mtemvu hayupo pichani.

Sitti A. Mtemvu akiwa katika Mahafali ya Shule za Sekondari Morogoro katika ukumbi wa Moro Sec. Mwenyekiti wa Sitti Tanzania Foundation 2015 Sitti A. Mtemvu akiwa na wanafunzi wa shule mbalimbali za Mkoa wa Morogoro wanaounda umoja wa Un Club Morogoro.

SITTI Abas Mtemvu mwenyekiti wa Sitti Tanzania Foundation (STF 2015) amepokelewa kwa shangwe katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Morogoro alipoalikwa katika mahafali yaliyofanyika katika ukumbi wa Shule hiyo baada ya kupokelewa na kundi la wanafunzi. Sitti alifika katika viwanja vya shule mapema akiambatana na mama yake mzazi Mariam Mtemvu, Kheri Mkamba katibu wa vijana mkoa wa Morogoro, wafanyakazi wa taasisi hiyo pamoja na wageni waalikwa . Akihutubia wanafunzi hao Sitti aliwaomba wanafunzi kutokata tama katika kujiendleza kimasomo kwani elimu ndio ufunguo wa maisha kwa kila mwanadamu, wawe na malengo ya kufika mbalia zaidi na isiwe kufika kidato cha sita ndio mwisho wa kusoma. “Dunia ya leo inahitaji sana Elimu hivyo si vema kwa mwanafunzi ambaye tunaye leo hapa kuona kuwa elimu ndio mwisho wake, no someni kwa bidii mfike vyuo vikuu na kupata shahada za juu,”anasema Sitti. Mwenyekiti huyo kupitia taasisi yake ametoa kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya kuchangia Un Club Tanzania Network Morogoro Cluster ambayo ndio kiungo kikubwa cha wanafunzi wa shule za Sekondari za Mkoa wa Morogoro. Maafali hayo yaliyoandaliwa na shule nne yalijumuisha pia shule nyingine tano wakiwaunga mkono wanafunzi wa kidato cha sita ambao ndio walikuwa wenye shughuli hiyo, shule zilizounga na kufanya sherehe pamoja ni Shule ya Sekondari ya Morogoro wenyeji. Shule nyingine ni Shule ya Sekondari Kilakala, Shule ya Sekondari Dakawa, na Shule ya Sekondari ya Mzumbe huku shule za Sua, Sekondari ya Mgulasi, Sekondari ya Sumaya, Sekondari ya Mafiga na Sekondari ya Uwanja wa Ndege zikishiriki katika tukio hilo la kihistoria. Taasisi ya Sitti Tanzania Foundation inatarajiwa kuzinduliwa rasmi tarehe 2- May- 2015 katika ukumbi wa Mlimani City, ni siku ambayo mrembo huyo amehaidi kuandika historia kubwa katika maisha yake kwani itakuwa ni sehemu kubwa kutimiza ndoto zake. Sherehe hizo zilipambwa na show kutoka kwa wanafunzi wenyewe ambao walionyesha vipaji katika uchezaji wa muziki na kuimba.

ABD Mcee ft Spac Dawg-MC (NOIZ)

Tuesday, March 17, 2015

UJIO MPYA WA PAH ONE "KIZUBANETA"

LINEX FEATURING DIAMOND PLATNUMZ - SALIMA

HATIMAYE LINEX AACHIA WIMBO WAKE MPYA SALIMA AKIMSHIRIKISHA DIAMOND PLATNUMZ

Linex akimshirikisha Diamond Platnumz katika wimbo wake mpya Salima ambao siku chache zilizopita ameuachia katika media mbalimbali. Video na audio ametoa kwa pamoja, Linex anaonekana kutulia sana katika wimbo huu, kama kawaida yake ametumia lugha 3 ndani ya wimbo, amepanga mashairi mazito yenye hisia na utunzi na ghani za mashairi yamepangiliwa katika ubora wa aina yake, lugha imetumika kiufasaha. Wimbo ni mzuri kwa ujumla ukiusikiliza hasa pale Diamond Platnumz alipofuata nyayo za uimbaji wa linex……….. ametumbukiza maneno ya kilugha kama afanyavyo Linex katika kila nyimbo zake anazoimba. Diamond ameutendea haki wimbo huu, wimbo unagusa nyoyo za watu…..wimbo unagusa hisia……na tena wimbo unaweza ukakutoa machozi..! welldone Linex….welldone Diamond….welldone team nzima na management inayomsimamia Linex kufanikisha kuutoa wimbo huu Video ya wimbo huu inavutia sana, pongezi kubwa sana kwa aliyeandaa siclipt ya video hii kwa kuweza kuindaa katika kiwango cha kutazamika kwa kila rika, video hii……natumaini inaweza kutumika na baraza la mitihani ya taifa ya kidato cha nne ama cha sita kuwatengenezea maswali kwa somo la Kiswahili….sitashangaa nikiona wimbo wa salima wa linex ikiwa mojawapo ya maswali ya mtihani wa ngazi ya taifa, its fantastic video! Miongoni mwa video zinazotarajia kufanya vizuri zaidi hasa nje ya nchi kwani ni video inayoonyesha uhalisia wa kitanzania kabisa hakika Linex pamoja na Diamond Platnumz wamefanya kazi kubwa na wavutia kwenye hii video, Pongezi za ziada ziende kwa AJ ( huyu ni Adam Juma) amefanya kazi ya ziada kwa kushuti kwa ustadi wa hali ya juu video hii…..kwakweli naweza kusema hii ndio video bora kwangu kwa mwaka huu 2015 ingawa mwaka haujaisha.

Sunday, March 15, 2015

SIKU YA YA MWISHO YA NOTISI KANISA LA MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA KUHAMA KAWE

9 MACHI 2015 SIKU YA MWISHO YA NOTISI KANISA KANISA LISILO RASMI KUHAMA KAWE Siku 30 za notisi zimetimia Mchungaji Josephat Gwajima Kufunga virago Kawe!


Kanisa la lisilo rasmi la mchungaji Mchungaji Josephat Gwajima lililokuwa likiendesha shughuli zake kinyume na taratibu katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe,wilaya ya Kinondoni,jiji Dar limeamuriwa kuondoka mara moja na kuwacha eneo hilo wazi kwa ajili ya maendeleo ya watu wa kawe. Kanisa hilo ambalo kwa muda mrefu lemekuwa likiendesha shughuli zake kinyume na taratibu na kusababisha usumbufu na kero kubwa za makelele kwa wakazi wa maeneo hayo. Katika Barua iliosainiwa na Meneja wa Mkoa wa Kinondoni wa shirika la nyumba la Taifa imesisitiza kwamba pamoja na kutambuliwa umuhimu wa kanisa hilo kuendesha shughuli zake lakini shirika hilo halitaweza kutoa ruhusa kwa kanisa hilo kuendelea kufanya mahubiri katika viwanja hivyo,kwani shirika hilo limeshaanza kutumia Viwanja hivyo kwa maendeleo ya wananchi wa KAWE ikiwa ni ujenzi wa makazi n.k Bw Masika ametoa siku 30 tu ambazo leo 9 Machi 2015 Mchungaji Gwajima anatakiwa kufunga virago na kuwacha viwanja hivyo wazi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi. Mchungaji Josephat Gwajima afunge virago

Friday, March 13, 2015

Rama Dee-Usihofie Wachaga


Seenga S ft Top G-Pombe Kiasi (NOIZ)

MKUTANO MAALUM WA WADAU WA FILAMU ZA MAADILI


MKUTANO MAALUM WA WADAU WA FILAMU ZA MAADILI WASANII,WATAYARISHAJI, WASAMBAZI,WATAMAZAJI NA WAANDISHI WOTE MNAKARIBISHWA

Asalaam Alaaikum Warhmatullah Wabarakatuhu Tunapenda kuwajulisha wadau wa maadili movies nchini kutakuwa na mkutano wa mkubwa utakaofanyika tarehe 31 Mai 2015 kuanzia saa 2.00 asubuhi ukumbi wa Jaffar Complex uliopo Mnazi mmoja jijini Dar es salaam

AGENDA ZA MKUTANO

Kuandaa daftar la orodha ya wasanii na kuchagua rasmi aina ya mfumo wa filamu zetu na mengineyo Kuchagua uongozi wa wa muda uliona mpangilio rasmi na kuupa majukumu likiwepo la Kuanzisha mtandao wenye hamasa na mwelekeo kwa wassii wote wa maadili Africa mashariki na Africa kwau ujumla Kushirikiana na kujenga na kuunga mkono kuimarisha soko la filamu Tunapenda kuaalika waandishi wa habari watunzi waongozaji wasambazaji na hata watazamaji wa filamu za maadili wasanii wote nchini tunawaalika ila stara ya mavazi kwa wanawake izingatie muhimu kwa wanawake "Maadili Movies Lengo ni kusimamia ulinzi wa maadili mema kupitia filamu za Kitanzania, kuazisha, kuendeleza na kuhamsisha uwepo na ukuwaji wa filamu zenye heshima, zinazozingatia maneno, matendo na mavazi yenye maadili." Tuwe pamoja wana
BURUNDI
RWANDA
KENYA
UGANDA
CONGO
TANZANIA na AFRICA KWA UJUMLA
Kwa mawasiliano ya simu kwa wale watakaoshiriki kutoka nchi tofauti tofauti pamoja na nchini ,Tafadhali tuwasiliane kwa simu kwa namba zifutazo: 00255 773 950 250 00255 715 305 528 00258 878566 042 00255 783 70 77 06
http://www.maadilimovies.blogspot.com

Double H-Naweka Nia (NOIZ)

NGOMA AFRICA BAND LIVE ! in STUTTGART on14 March 2015 Africa Unite PartyClick to teach Gmail this conversation is important.


ALL AFRICAN AND FRIENDS OF AFRICA ARE INVITED TO ATTEND THE AFRICA UNITE PARTY ON THE 14.MARCH 2015 IN STUTTGART. LIVE ON STAGE NGOMA AFRICA BAND

RAMBI RAMBI ZA NGOMA AFRICA BAND KUFUATIA MSIBA WA JOHN KOMBA

NGOMA AFRICA BAND YAUNGANA NA WATANZANI KATIKA MAOMBOLEZO

YA MAREHEM JOHN KOMBA (RIP)

Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya the Ngoma Africa band yenye maskani yake nchini Ujeumani inaungana na ,watanzania wote popote pale katika kipindi hiki cha msiba wa mwanamuziki marehemu John Komba (RIP) ,marehemu

alikuwa muasisi wa Kikundi cha muziki cha TOT,muhamasishaji,tutamkumbuka daima kwa mchanngo wake wa kuelemisha jamii kwa njia ya muziki.Ngoma Africa band inawapa pole ndugu na familia yote ya marehemu,pole na rambi rambi pia

ziwafikie TOT,Wapiga kura wa jimbo lake la Mbinga magharibi.Spika wa Bunge na bunge lote la Tanzania,marafiki,Uongozi na Chama Tawala CCM,wanamuziki na

watanzania wote, tupoe sote kwa msiba huu wa mwanamuziki Marehemu Kaptani

John Komba (RIP) mwenyezi mungu amlaze mahala pema.

Rambi rambi kutoka

Ngoma Africa Band

Oldenburg, Germany


The Ngoma Africa Band

www.ngoma-africa.com

KAZINDA-Danny Pes

New Video : Vitamin Music - Belle 9 ft Joh Makin

Kama bado hujapata video mpya ya Belle 9 aliyomshilikisha Joh Makin itwayo Vitamin Music iangalie sasa kwa kuifata link YouTube, Mastaa wengine walioonekana kwenye video hii ni pamoja na JOTI wa Zekomed anaonekana akiudumia wagonjwa wenye ukosefu wa VITAMIN MUSIC Hospital na kwa kunogesha pia anaonekana Rapa Young Dee. “Belle 9 Featuring Joh Makini - Vitamin Music Official Video” — Produced by Mona Gangstar - Classic Sound Directed by Khalfan Bamushka

FID Q-Bongo HipHop (Official Video)

Top In Pemba-Yameniumiza Sana (NOIZ)

"Top In Pemba" aachia wimbo wake "Yameniumiza Sana" toka @noizmekah chini ya @defxtro

Bad Breakers-Bila Wewe (DraRecs.Noiz)

Bofya HAPA http://goo.gl/TsFz2H Download wimbo wa Bad Breakers "Bila Wewe" ikiwa ni mkono toka kwa producer Dra wa DRA Recs Monduli na vocals pande za Noizmekah chini ya Defxtro

Hone Classic-We Mama (NOIZ)

Leikiz ft Ordinally JamboSquad-Bounce Like This (NOIZ)

Bofya HAPA https://mkito.com/song/bounce-like-this-ft-ordinally/13296 kupakua wimbo wa "Leikiz featuring Ordinally wa Jambo Squad" kwa jina "Bounce Like This" ikiwa ni HipHop Bounce category toka @noizmekah chini ya @defxtro

Wednesday, March 11, 2015