Tuesday, July 26, 2016

Serikali ya Congo yachukua maamuzi mazito baada ya Koffi Olomide kurudi

Mwanazmuziki mkongwe Koffi Olomide ambaye alikuwa nchini Kenya julai 22 akiwa na wanamuziki wake pamoja na madensa wake watatu kwa ajili ya show alioatakiwa kuifanya siku ya jumamosi julai 23 wakati aliposhuka uwanja wa ndege wa Jomo Kenyata alimpiga densa mateke densa wake wa kike.

Leo julai 26 2016 ya Congo imemtia hatiani mwanamuziki huyo baada ya kuwasili kutoka nchini Kenya na kuhukumiwa miezi kumi nane jela.

Olomide amekuwa na makosa yanayofanana siku za nyuma

Mwaka 2012 aliwahi kuingia hatiani baada ya kumpiga producer wake na kuhukumiwa miezi mitatu jela.

Mwaka 2008 alimpiga camera man wa RTGA television na kuvunja camera yake katika tamasha mjini Kishasa.

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako/ Leave your comments