Wednesday, July 18, 2012

HILI NI ENEO MAALUM LILILOANDALIWA KWA AJILI YA WATU KWENDA KUTAMBUA MIILI YA NDUGU ZAO

Sehemu ya kuhifadhia miili ya marehemu kwa ajili ya watu kwenda kuwatambua ndugu zao ikifanyiwa maandalizi katika viwanja vya maisara
Umati wa watu wakiwa pembezone mwa bahari maeneo ya maisara wakiangalia boat za uokoaji zikirejea bandarini
Askari wa kikosi cha KMKM wakishirikiana na kikosi cha msalaba mwekundu kuipanga miili ya marehemu sehemu maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya watu kupita kutambua miili ya ndugu zao
Baadhi ya miili ya marehemu iliyotangulia kuletwa eneo hili maalum kwa ajili ya kutambuliwa na ndugu zao
Tulipokuwa katika viwanja vya maisara na waandishi wenzangu kutoka kushoto ni Lazaro Philipo Matarange, Hussein Hamis Mgonanze na Mbaraka Said Boha.

Mpaka muda tulioondoka katika eneo hili ilikuwa jumla ya maiti 7 zimewasilishwa, maiti 3 za watoto na maiti 4 za wakubwa wakiwemo wanawake 2 mmoja ni mzungu ambae ni mgeni alikuwa na wenzake saba wameokolewa na wanaume 2. Kwa upande wa watoto haikuweza kufahamika kwa haraka jinsia zao. Kwa upande wa majeruhi walikuwa 24 akiwemo mtoto 1.

Kwa taarifa zaidi sikiliza Coconut Fm kwa wewe ambaye unaishi Ungunja kwa uliye mbali endelea kufuatilia kpitia blogg hii. Pia naomba radhi kwa picha ambazo hazikustahili kuwekwa humu.

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako/ Leave your comments