Thursday, July 19, 2012

SHUGHULI ZA UOKOAJI ZINAENDELEA ...WATU WAENDELEA KUSUBIRIA MAITI ZINAZOENDELEA KUPELEKWA KATIKA VIWANJA VYA MAISARA

Watu wakiendelea kusubiria kutazama maiti zainazoendelea kuletwa


Watu wakiwa kwenye mstari wakiingia sehemu ilipohifadhiwa maiti kwa ajili ya kutambua ndugu zao
Vikosi vya maafa wakishusha miili iliyopatikana leo

Hivi ndivyo hali ilivyokuwa mchana wa leo katika viwanja vya maisara watu ni wengi wakiendelea kusubiria maiti zinazopelekwa hapo kwa ajili ya kutambuliwa na ndugu zao.

Mpaka kufikia asubuhi ya leo maiti 30 zilipatikana ambapo kati ya hizo 20 zimetambuliwa na kuchukuliwa na ndugu zao na watu 145 wameokolewa wakiwa hai hii ni kwa taarifa kutoka mamlaka ya serikali.

Wakati shughuli za uokoaji zinaendelea leo mpaka kufikia jioni hii maiti 30 zimepatikana na kupelekwa katika viwanja vya maisara ambapo watu bado wanaendelea kupita kutambua ndugu zao.

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako/ Leave your comments